UTANGULIZI
Choroko ni zao la chakula na biashara lenye kiasi kikubwa cha protini na madini
ya phosphorus na calicium.Zao hili likilimwa vizuri hutoa mavuno kati ya Kg 400
hadi 900 kwa ekari.
UDONGO NA HALI YA HEWA IFAAYO.
Choroko hustawi katika udongo wa aina tofauti tofauti usiotuamisha maji.Hulimwa
kutoka mita 0 hadi 1500 kutoka usawa wa bahari japokuwa kuna mbegu nyingine
zinaweza kukubali zaidi ya ukanda huu.Hili ni zao linalostahimili ukame.
AINA ZA CHOROKO
Kuna aina kuu mbili za choroko ambazo pia zimegawanyika katika makundi
mawili,choroko nyeusi na choroko za kijani.
1>CHOROKO ZINAZOTAMBAA-hizi ni choroko ambazo zinarefuka sana na
hutambaa sehemu mbalimbali.
2>CHOROKO ZINAZOSIMAA=Hizi ni choroko ambazo zinakuwa kwa kusima
kwenda juu.Hizi huchukua muda mfupi kukomaa wastani wa siku 60-70
Choroko hazihitaji maji mengi hivyo ni budi zipandwe mwishoni mwa msimu wa
mvua,Pia zinaweza kupandwa katika shamba lililolimwa mpunga.
NAFASI ZA UPANDAJI WA CHOROKO NA KIASI CHA MBEGU
Choroko huitaji mbegu kiasi cha kilogram 8 hadi kumi kwa ekari moja.
Panda choroko zako kwa nafasi ya sentimeta 30 mastari na mstari na sentimeta 10
shina hadi shina (30 x10 )sentimeta au (40 x 8 )sentimeta
SAMADI NA MBOLEA ZA VIWANDANI
Kama shmba lako halina rutuba ya kutosha unaweza kuongeza samadi kiasi cha tani
tano kwa ekari na pia unaweza kupanda kwa kutumia mbolea ya NPK kg 50 kwa
ekari.weka mbolea zote kabla ya kupanda.
UMWAGILIAJI
Kama umepanda kipindi cha ukame sana au unalima kilimo cha umwagiliaji basi
mwagilia shamba lako upate unyevu wa kuotesha mbegu, kisha baada ya mbegu kuota
kaa siku 6 hadi 10 na umawgilie tena. Mara tatu za kumwagilia zinatosha kwa
choroko.
PALIZI
Palilia shamba lako mapema kuzuia magugu.Palizi moja inaweza kutosha.
MAGONJWA YA CHOROKO
1-yellow mosaic virus ( Ugonjwa wa manjano)
Dalili- mmea unakuwa wa njano na madoa ya njano katika majani.
Kinga na tiba-Panda mbegu zinazostahimili magonjwa.
2-Powdery Mildew (Ukungu)
Dalili-Majani yanakuwa na vidoti vya njano ambavyo vinabadilika kuwa vya
kahawia au kijivu haraka na ambapo kunakuwa na unga unga katika majani.
Kinga na tiba-Panda mbegu zinazostahimili ukungu,Pulizia dawa za ukungu
(Fungicide).
anza kupuliza wiki tatu baada ya mimea kuota na kuendelea kulingana na hali
halisi.
3> LEAF SPOT (Vidoti katika majani)
Dalili-majani yanakuwa na vidoti vya mviringo na visivyo na umbo maalum ambapo
katikati yanakuwa na rangi rangi ya kijivu na weupe na mistari ya rangi ya
wekundu-kahawia au nyeusi-kahawia.ugonjwa huu husababisha hasara hadi ya
asilimia 58 ya mapato.
Kinga na Tiba-Panda mbegu inayostahimili ugonjwa huu,Choma mabaki ya mimea hii
na ile ya jamii moja baada ya kuvuna.Pulizia dawa za ukungu (Fungicide) Katika
nafasi ya wiki mbili mbili kama eneo hilom linashambuliwa mara kwa mara na
ukungu
WADUDU.
Kuna wadudu mbalimbali wanaoshambulia choroko kama vile aphidi,funza wa
vitumba,nzi wa maharage.Wazui wadudu hawa kwa kupuliza dawa za wadudu mara tu
baada ya mimea kuota,dawa kama karate,twigathoate,dimethote na nyinginezo
zinaweza kutumika.
UVUNAJI
Mara tuu choroko zinapofikia asilimia 85 ya ukaukaji zinabidi zivunwe
ukichelewa zitapukutikia shambani...Kwa Ushaur zaidi piga simu namba 0718405318
kutana idara makini ya washauri hapa (KMT )Kilimo na mkulima Tanzania