About Me

Morogoro, Morogoro mjini, Tanzania

Tuesday 27 December 2016

FAHAMU MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA HUJAINGIA KATIKA KILIMO CHA BIASHARA.

Kabla haujaamua kuingia katika kilimo cha biashara inakupasa kwanza ufahamu mambo muhimu ambayo yatakusaidia katika shughuri yako ya kilimo husika.Kwani yakupasa kutambua kila kazi ya kuingiza kipato ina changamoto zake na kilimo ni moja ya kazi yenye changamoto nyingi ambazo yakupasa nyigine ujipange jinsi ya kukabiliana nazo kabla ya kuaingia katika kilimo husika.
Mambo hayo muhimu ni
https://scontent-lhr3-1.xx.fbcdn.net/v/t1.0-9/15589485_435477463507837_2393623494652658756_n.jpg?_nc_eui2=v1%3AAeFiqJH6z1PMfQ0kf8FeUW5XX_Q0C2x0uONTj89jeqT2E3_1KzAW853uhWIJoYb4nYn4jEVlL2tqIyoDzWnSF2YgtL6odwSBR9ij67YoC-_dxwYVkzpLFvT3xUXhXGX4uMI&oh=9ed32f8c57961d99f9af4cd1081ce803&oe=58DC7DB7
1>UTAYARI KUINGIA KATIKA KILIMO
Inakupasa kabla hujajiingiza katika kilimo uwe tayari wewe mwenyewe kuamua kuanza kufanya kufanya kilimo husika,Kwa maana nyingine namaanisha maamuzi yako ya kuingia katika kilimo yatokane na uchaguzi wako mwenyewe baada ya kuangaliaya na kuona kilimo ni moja ya jambo litakaroboresha kipato chako.Ili kuepuka kujiuliza uliza maswali ya uamuzi wako wa kwanini na nani amekushauri kuingia kufanya shughuri hiyo ya kilimo husika,Hivyo utayari wako utakusaidia kuongeza ari na juhudi zaidi katika kazi yako na kukupunguzia kukata tamaa njiani.

2>UCHAGUZI WA KILIMO KINACHOKUFAA
Kabla ya kuingia katika kilimo lazima kwanza ufanye uchaguzi wa kilimo gani ambacho utafanya.Katika Uchaguzi lazima uchague kitu ambacho utakuwa tayari kukifanya bila kupata pingamizi la utayari wa kufanya kilimo hicho.Katika uchaguzi unaweza kuchagua kilimo mchanganisho kwa maana kulima mazao na kufuga mifugo au kulima mazao/kufuga mifugo tuu.
Na hapa katika uchaguzi ukichagua kilimo ambacho si sahihi kwako ndipo ambapo husababisha changamoto nyingi katika kilimo chako hapo baadaye.Hivyo uwe makini katika kuchagua Mazao/Zao,Mifugo/Mfugo sahihi kwako kutokana na utakavyojiangalia utayari wako.Pia suala la uhakika wa uwepo wa soko la utakachochagua kukifanya ni kitu cha msingi katika kilimo chako,Kwani yakupasa utambue hapo baadaye utahitajika uuze ulichozalisha hivyo usipokuwa makini inaweza kusababisha hasara kubwa katika kilimo chako.Na yakupasa kutambua kuwa bei hubadilika badilika kulingana na msimu wa mavuno na bei za soko.

3>UTAFITI NA USHAURI WA GHARAMA JUU YA KILIMO ULICHOKICHAGUA
Baada ya kufanya uchaguzi wako inakupasa ufanye utafiti wa gharama utakazoweza kuzimudu katika kilimo chako.Hili litaendana na Ushauri wa Jinsi gani ya kuweza kufanya kilimo chako kwa gharama nafuu zaidi ili kama ikitokea hasara uwe na uwezo wa kuikabili vizuri.

4>PANGA BAJETI YAKO KABLA HUJAANZA KILIMO
Yakupasa upange bajeti yako kabla hujaanza kilimo kwa kuangalia utafiti na ushauri wa gharama juu ya Kilimo ulichokichagua.Hi itakusaidia katika manunuzi na malipo ya huduma muhimu katika shughuri zako kwani utakuwa umejipanga mapema kukabiliana na matatizo yatakayohitaji fedha ya mfukoni kwa ajili ya huduma kama madawa,mbegu n.k
Kumbuka* malipo ya watakaohudumia kilimo chako usiyasahau katika bajeti yako na yataendana kulingana na idadi ya utakaowaajiri.

5>USIMAMIZI MZURI
Baada ya Kupanaga mipango yako usisaha katika kupanga vizuri usimamizi wa kilimo chako na hapa ukifanya makosa kamwe hutoweza kufanikiwa na kuishia kukiona kilimo hakifai hata kama ulitoa gharama zote zilizohitajika wenyewe wanasema uchungu wa mwana ajuaye mzazi,,wakulima tunasema uchungu wa kilimo aujuaye mkulima,Msemo huu,hii ianamaanisha uangalizi wako kwa ukaribu katika kilimo chako unahitajika zaidi kuliko kuwa mtu wa kuagiza tuu bila kufuatilia maendeleo ya kilimo chako wakati kinafanyika.

6> TAFUTA USHAURI WA UTAALAM WA KILIMO ULICHOKICHAGUA
Kabla hujaanza usisite kutafuta ushauri wa kitaalam wa kilimo ulichokichagua.Ili uwe karibu na kugundua tatizo katika kilimo chako kabla hujachelewa sana kupata athari ya tatizo husika.Na pia hili litakusaidia kufanya kilimo chako kwa uhakika zaidi.

7> ANZA KILIMO CHAKO KWA UHAKIKA
Mwisho baada ya kupitia hatua hizo juu anza kufanya kilimo chako kwa uhakika zaidi na Pia huku unatambua kilimo nacho ni biashara kama zilivyo biashara nyingine hivyo uwe makini katika kilimo chako ili kujiepusha na changamoto zitakazojitokeza katika kilimo chako na changamoto hizo zisiwe kikwazo katika kukuzuia kuendendelea na kilimo chako.. EPUKA UMASIKINI KILIMO NI PESA.WASILIANA NASI KUPITIA NAMBA 0718 405318 AU 0767405318

No comments:

Post a Comment