About Me

Morogoro, Morogoro mjini, Tanzania

Tuesday 27 December 2016

NAMNA BORA YA KUSINDIKA NYANYA

https://scontent-lhr3-1.xx.fbcdn.net/v/t1.0-9/15094883_417356921986558_356636340443847665_n.jpg?_nc_eui2=v1%3AAeHq1bcpjJ19qpvN_G1LnFRfNtJYHUGfIxlpNFBaixvAwvO58LuBzFjmBQc_-lOWiXjothg4e4tz1SeBe3hXJQrIzTmjBk835Xh0DxdexTMp8mSDMRL8CRUXzNu7J5bjksQ&oh=5662250edc17a25cc8335156904fc4ef&oe=58E15143
Nyanya zinaweza kusindikwa kupata bidhaa mbali mbali ili kuepuka uharibifu wa zao, kuongeza ubora na thamani, na pia kuwezesha upatikanaji wake wakati wote.
Baadhi ya bidhaa zinazotokana na zao la nyanya ni kama vile nyanya za kukausha, Juisi, pesti au lahamu na sisi au urojo.


1. KUSINDIKA NYANYA KWA KUKAUSHA
Nyanya za kukausha zinatakiwa ziwe zimekomaa na kuiva vizuri. Aina ya nyanya zinazopendekezwa kukausha ni zile zenye Nyama nyingi kama vile Tengeru 97, Roma na Tanya.

VIFAA
Visu vikali visivyoshika Kitu, ungo, sufuria, Jiko, kaushio bora, mifuko ya plastiki na beseni.

MALIGHAFI
Nyanya zilizokomaa na kuiba vizuri na ngumu, Maji safi na Salama.

JINSI YA KUKAUSHA
Chukua nyanya zilizokomaa na kuiba vizuri kisha OSHA kwa Maji safi na Salama.
Kata nyanya katika vipande vyenye Unene wa wastani usiozidi milimita Tano kwani Unene ukizidi vipande havitakauka vizuri na Kupungua ubora.
Panga nyanya kwenye kaushio safi ili zikauke.
Wastani wa kilo moja ya nyanya unaweza Kutoa gramu 180 za nyanya zilizokaushwa.
Fingasha vipande Vya nyanya vilivyokaushwa kwenye mifuko safi isiyopitisha unyevu.
Weka Lebo na hakikisha lebo inaonesha muda wa kisha kwa matumizi kuwa Mwaka Mmoja kutoka Siku ya kutengenezwa.
Hifadhi kwenye sehemu yenye ubaridi na kavu.

MATUMIZI
Nyanya zilizokaushwa hutumika kama kiungo kwenye Vyakula mbali mbali.

2. KUSINDIKA NYANYA KUPATA JUISI
Nyanya kama matunda mengine huweza kusindikwa na kutengenezwa Juisi ambayo hutumiwa na watu wa rika zote.

VIFAA
Chupa zenye mifuniko imara, lebo, chujio au kitambaa safi, sufuria, ndoo au beseni, kisu kisichoshika Kitu, mizani na Mashine ya Kusaga nyanya.

MALIGHAFI
Nyanya zenye Juisi nyingi kama vile marglobe, money maker, Sukari nyeupe na chumvi.

JINSI YA KUTENGENEZA JUISI
Chagua nyanya zilizokomaa na kuiba vizuri kisha osha kwa Maji safi na Salama.
Katakata nyanya katika vipande kidogo kisha Pima uzito wa nyanya.
Kwa kilo moja ya nyanya, ongeza Maji kiasi cha Lita moja.
Chemsha kwenye moto wa kadiri (nyuzi moto 85 za sentigredi) kwa muda wa dakika 5.
Saga nyanya kwa kutumia Mashine ya mkono au Umeme kisha chuja rojo ili kupata Juisi.
Pima uzito wa Juisi na ongeza Sukari gramu 20 na chumvi gramu 10 kwa Kila Lita 1 ya Juisi.
Chemsha tena kwenye moto wa kadiri (moto la nyuzi 85 hadi 90 za sentigredi) kwa dakika 20.
Ipua Juisi na jaza Juisi Ikiwa ya moto kwenye chupa safi zilizochemshwa kisha zifunike na zipange kwenye sufuria.
Weka Maji ya uvuguvugu kwenye sufuria hiyo hadi yafike nusu ya kimo cha chupa kisha chemsha tena chupa hizo ili kuondoa hewa iliyopo Ndani ya chupa za Juisi na kuua vijidudu.
Ipua na acha zipoe, kisha weka lebo na lakiri.
Hifadhi kwenye sehemu yenye ubaridi safi na mwanga hafifu.
Juisi ya nyanya iliyotengenezwa kwa Njia hii huweza kuhifadhika kwa muda wa miezi Sita bila kuharibika.

MATUMIZI
Hutumika kama kiburudisho na hutupatia virutubisho vingi mwilini.
Virutubisho vinavyopatikana katika gramu 100 za Juisi ya nyanya ni kama ifuatavyo;
Maji. 94%
Wanga. 4.3g
Sukari. 3g
Madini ya Chuma 0.6g
Vitamini C. 61.7ml
Nguvu. 92 Kilokari
Vitamini A. 74 I.U

3. KUSINDIKA NYANYA KUPATA LAHAMU AU PESTI

VIFAA
Jiko, mizani, kisu kisichoshika Kitu, sufuria, chupa zenye mifuniko imara, lebo, Mashine ya Kusaga, meza ya Kukata na chujio.

MALIGHAFI
Nyanya zinazotoa rojo nyingi kama vile Roma na Tanya, wanga wa Mahindi, ndimu ya Unga, sodium benzoate na chumvi.

JINSI YA KUTENGENEZA
Chagua nyanya zilizokomaa na kuiva vizuri kisha osha kwa Maji safi na Salama.
Kata nyanya katika vipande kidogo kisha chemsha hadi ziwe lakini.
Chuja kupata Uji mzito na ondoa Maganda na mbegu.
Pima uzito wa pesti na weka chumvi gramu 40 kwenye kilo moja ya pesti.
Chemsha ukiwa unakoroga hadi pesti ibaki nusu.
Ongeza wanga utokanao na Mahindi kiasi cha gramu 20, ndimu ya Unga gramu 5 na mikrogramu 800 za sodium benzoate kwa kilo moja ya pesti.
Chemsha kwa muda wa dakika Tano na weka kwenye chupa Ikiwa bado ya moto.
Panga chu

pa zenye pesti kwenye sufuria na weka Maji kwenye sufuria hiyo hadi yafike nusu na kimo cha chupa.
Chemsha chupa hizo kwa muda wa dakika 20 ili kuondoa hewa na kuua vijidudu.
Ipua, acha zipoe kisha weka lebo na lakiri na kuhifadhi kwenye ubaridi.
Pesti iliyotengenezwa kwa Njia hii huweza kuhifadhiwa kwa muda wa miezi Sita bila kuharibika.

MATUMIZI
Pesti ya nyanya hutumika kama kiungo cha chakula na aina ya virutubisho vingi.
Virutubisho vinavyopatikana kwenye gramu 100 za pesti ya nyanya ni kama ifuatavyo;

Nguvu. Kilokari 442
Wanga. Gramu 19.6
Protini. Gramu 4.4
Maji. Gramu 75
Vitamini A. Miligramu 330
Vitamini C. Miligramu 17.8
Potasiamu. Miligramu 888
EPUKA UMASIKINI KILIMO NI PESA 0718405318 au 0767405318

No comments:

Post a Comment